Moja mbili tatu kimbia!

“Wacha tucheze mchezo wa kujificha na kutafuta. Unahesabu hadi kumi na nitajificha,” akasema Kim na kufunga macho yake na Rita akajificha. Alikimbia nyuma ya mti na kuweka nguo yake ya machungwa na ndizi nyuma yake. Aliinamisha kichwa chini. Nywele zake za kahawia nyeusi ziligusa ardhi.

Alicheka huku akimsikia Kim akizungukazunguka akimtafuta. We! Wee! Wee! Akaiinua kichwa chake na kuchungulia. Wakati huo huo, Kim alitua kwenye mti, mbele ya Rita. “Umenipata,” akatabasamu.

“Ni zamu yangu ya kuhesabu. Jifiche na nitakupata,” alisema. Kim akaruka juu ya shina la mti lenye shimo na kuruka ndani. “Nimekuja,” Rita aliita na kuanza kumtafuta rafiki yake. Alitazama nyuma ya mti wa mwaloni. Alitazama juu ya miti.

Aligawanya majani marefu, yenye kutikisa na kutazama. Kim hakupatikana popote. “Nashangaa amejificha wapi?” Akasikia kelele. Ilisikika kama mcheko wa Kim. Alikimbilia kwenye shina la mti na kuchungulia ndani. “Kuna wewe. Nimekupata,” akaita


	

Taji ya maajabu

Tumbili walishangaa kuona miti ikipungua. Jua likiwaka liliwapiga bila huruma kwa sababu hapakuwa na kivuli.

Adui zao waliwaona kwa urahisi kwa sababu hapakuwa na mahali pa kujificha.

Wanyama wakafanya mkutano na kumtuma mfalme wao apate kujua mahali miti yao inapotelea.